Pages

Subscribe:

Thursday, 22 January 2015

RAGE ATAKA FURSA KWA WACHEZAJI WA TANZANIA

KIONGOZI wa zamani wa klabu ya SIMBA na shirikisho la soka nchini TFF , ISMAIL ADEN RAGE amevitaka vilabu vya soka nchini kuwa na mipango endelevu hasa kwa wachezaji wa hapa nyumbani ili waweze kucheza nje ya nchi.

RAGE ameyasema hayo baada ya mshambuliaji wa TP MAZEMBE, MBWANA SAMATTA kupata fursa ya kwenda kufanya majaribio katika klabu kubwa ya RUSSIA ya CSKA MOSCOW.


MBWANA ni miongoni mwa wachezaji wanaofanyiwa majaribio na klabu hiyo ya CSKA MOSCOW ambayo hushiriki katika michuano mikubwa ya vilabu barani Ulaya.

Wakati akiwa mazoezini MBWANA aliumia enka na hivyo hakucheza mchezo kati ya CSKA MOSCOW na SION ya USWISI ambayo SION ilifungwa goli MOJA kwa BILA.


0 comments:

Post a Comment