Pages

Subscribe:

Thursday, 22 January 2015

TAIFA STARS MABORESHO YATOKA SARE NA AMAVUBI


Kitoka Mwanza 

TIMU ya taifa ya maboresho ya TANZANIA imecheza mchezo wake wa kimataifa wa kirafiki na Amavumbi ya RWANDA kwenye uwanja wa CCM KIRUMBA MWANZA.

Kocha Mart Nooj
Katika mchezo huo dakika ya tisa RWANDA waliweza kupata goli kupitia kwa mchezaji JEAN BATISTA MUNGIRANEZA.

TAIFA STARS maboresho iliweza kusawazisha goli hilo katika dakika ya 43 ya mchezo kwa goli lililofungwa na FRIDAY KELVIN baada ya kupokea pasi kutoka kwa SIMON MSUVA.

Timu zote zinajiandaa na mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza timu za mataifa yao na ligi za nyumbani kwao yaani CHAN.


RWANDA ni mwenyeji wa mashindano ya CHAN yatakayofanyika mwakani, huku TANZANIA ikijiandaa na michezo ya kutafuta tiketi ya kucheza michuano hiyo.

0 comments:

Post a Comment