Pages

Subscribe:

Wednesday, 21 January 2015

TAMBWE- NIMEAMBIWA MANENO YA KIBAGUZI



 YANGA YATAKA ADHABU SAKATA LA AMIS TAMBWE

    TAMBWE- NIMEAMBIWA MANENO YA KIBAGUZI 


KLABU ya YANGA imeliomba shirikisho la soka nchini TFF kutoa uamuzi wa ugomvi aliofanyiwa mchezaji wao AMIS TABWE wakati timu yao ilipocheza na RUVU SHOOTING katika uwanja wa Taifa jijini DSM.

vurugu
Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano JERRY MURO amesema vitendo kama hivyo visipothibitiwa mapema italeta vuruge uwanjani.




Aidha YANGA imeomba TFF ikague ripoti za waamuzi na makamisaa ili kufahamu na kutokomeza vitendo vya fujo uwanjani kabla ya kutokea kwa vurugu kubwa.

AMISI TAMBWE ambaye aliibuka mfungaji bora msimu uliopita akiwa na timu ya SIMBA ameshangazwa na uchezaji wa kukabwa na akashutumu vikali maneno ya kibaguzi yaliyotolewa na mchezaji wa RUVU SHOOTING, GEORGE MICHAEL kwamba ni mkimbizi.


KOCHA wa Yanga, Hans Pluijm amekaririwa akisema kwamba kuna hujuma za kuwafanyia rafu na kuwaumiza makusudi wachezaji wake wanne kwenye mechi za Ligi Kuu Bara.

Wachezaji hao wanne ambao Pluijm amesema wanafanyiwa fujo na hujuma za waziwazi uwanjani ni Amissi Tambwe, Kpah Sherman na viungo wa pembeni Andrey Coutinho na Simon Msuva.



Pluijm amesisitiza kwamba hataki timu yake ipendelewe na waamuzi, lakini akawaonya waamuzi hao kuhakikisha wanaongeza umakini kugundua rafu wanazochezewa washambuliaji wao ambao wamekuwa wakikamiwa vibaya na timu pinzani.

0 comments:

Post a Comment